Tangu tukiwa watoto tumekuwa tukitamani kuitwa Baba au Mama, na hii imekuwa ikidhihirishwa kwa matendo na michezo.
Umri unavyosogea na matendo yetu juu ya tamanio letu juu ya uhitaji wa watoto umekuwa ukioneshwa kwa matendo mbalimbali
Hiyo yoote bado haijafanya jamii zetu ziwe salama dhidi ya : Utoaji mimba, Uaji wa Vichanga, na utupaji wa Watoto.
Matukio haya bado ni mwiba na yanatokea saana katika mitaa yetu,maana taarifa hizi zipo kila leo.
sasa Je :
Nini kifanyike ili kupunguza,kuzuia na kutokomeza matendo haya…..
Ni nini kifanyike kwa Waathirika wa Utoaji mimba,utupaji na Utelekezaji wa watoto wachanga….
Maoni na mtazamo wako ni muhimu katika kunusuru jamii zetu..
Ahsantee……
Suala la utoaji mimba ambalo halijaidhinishwa kiafya ni uuaji kama uuaji mwngne…Kimsingi mimba ikishatungwa si suala la kushtukiza baada ya miezi tisa…Me ninaloliona ni mmomonyoko wa maadili.Jamii imeacha mtizamo wa KIMUNGU imeegemea kwenye taarfa za makubaliano ya watu wachache…suala la ngono limepewa kipaumbele kuliko madhara kwa hyo jamii imechefukwa…la msingi ni turudi kwenye msingi wa KiMungu …
LikeLike